Monday, September 10, 2018

KILIMO CHA VITUNGUU MAJI

 
Aina za vitunguu
KILIMO CHA VITUNGUU
Utangulizi
Vitunguu maji hulimwa kama zao la biashara katika sehemu nyingi Duniani zenye hali ya hewani baridi ya wastani na joto kiasi.
Vitunguu ni zao la mbogamboga na hulimwa kwa ajili ya balbu zake. Tanzania vitunguu hulimwa sana sehemu za Mang’ula, Mgeta na Singida.
Hata hivyo vitunguu hustawi maeneo mengi ya Tanzania. Vitunguu vinaweza kulimwa mwaka mzima endapo maji yanapatikana.
Vitunguu vina matumizi mengi sana na vina madini joto, chuma, vitamin A, vitamin B, vitamin C na vitamin E
.
HALIJOTO
Joto linatakiwa sana kwa ajili ya ukuaji wa balbu ila joto likizidi vitunguu hukomaa mapema kabla balbu hazijafikia ukubwa unaostahili, hivyo mkulima anaweza kupata mazao kidogo.

AINA YA UDONGO
Vitunguu huweza kupandwa kwenye udongo wowote wenye rutuba,usiotuamisha maji na usionata sana.
Hufanya vizuri kwenye udongo wenye asidi kidogo japo udongo wenye alkali kidogo sio mbaya sana. Kwenye udongo wenye mchanga mchanga umwagiliaji ni lazima.
Udongo mzuri sana kwa ustawi wa vitunguu ni tifutifu-kichanga.
Umwagiliaji ni muhimu sana hasa wakati wa kuanza kutengeneza balbu. Unyevu uliozidi ni hatari sana kipindi cha ukuaji.
Epuka matumizi ya mbolea mbichi isioiva vizuri kwani husababisha vitunguu kuwa na shingo pana sana majani hukua sana badala ya balbu.



 UPANDAJI WA VITUNGUU
Kabla ya kupanda udongo ni lazima utifuliwe vizuri na reki kuondoa mabaki ya mimea na mawe ama Vipande vikubwa vya udongo. Matuta yawe na upana wa mita moja. Vitunguu hupandwa kwa mstari mojakwamoja ama kutokea kitaluni. Pia huweza kupandwa kwa mstari pacha. Vitunguu hupandwa sm 10-15 kutoka mmea hadi mmea na sm 10-15 kutoka mstari hadi mstari


EPUKA
Kununua mbegu za mitaani, kuzidisha sana mbolea na umwagiliaji usio na mpangilio kwani husababisha vinguu kuzaa pacha.
Pia epuka kupanda vitunguu mahali palipopandwa mboga jamii ya vitunguu siku za nyuma. Mfano Vitunguu saumu na vitunguu majani.

KITALU CHA VITUNGUU
Ni muhimu kumwagilia maji ya kutosha siku kumi za mwanzo tangu kusia mbegu kitaluni. Vitunguu hukaa kitaluni kwa wiki 6-8 na miche ifikiapo upana wa penseli na urefu wa sm 15 ni tayari kwa kuhamishia shambani/bustanini.

AINA ZA VITUNGUU VINAVYOLIMWA NCHINI TANZANIA
·         Red Creole
·         Bombay Red
·         Hybrid F1

UANDAAJI WA MBEGU
Uchaguzi wa mbegu bora ni muhimu sana katika uzalishaji miche yenye afya bora na yenye uzalishaji mazao mengi na yaliyo bora. Mbegu bora lazima ziwe na sifa zifuatazo;
1. Mbegu safi zisizo na mchanganyiko
2. Uotaji zaidi ya 80%
3. Chanzo sahihi cha uzalishaji mbegu
4. Tarehe ya uzalishaji mbegu isizidi mwaka mmoja
5. Chagua mbegu yenye soko kulingana na wakati
6. Hekta moja inatosha mbegu 3.5 hadi 4kg

UHAMISHAJI WA MICHE YA VITUNGUU KUTOKA KITALUNI KWENDA SHAMBANI
Zoezi la uhamishaji wa miche ya vitunguu hufanywa wakati miche imefikia umri wa wiki 7- 9.
Pia miche hiyo iwe imefikia unene wa shingo yakitunguu ukubwa wa 1/2 ya penseli au 3/4 penseli na wakati huo miche iwe imefikia urefu wa 15cm, Pia shina la kitunguu unapanda kwenye shimo lenye urefu wa 5cm.

NAMNA YA UTUNZAJI WA SHAMBA
Inashauriwa kutandazia shamba na majani yaliyooza vizuri ama mabua ili kuongeza ruba ya ardhi na pia kuzuia magonjwa yatokanayo na udongo na magugu. Kupanda vitunguu kwenye matuta yaliyoinuka ni muhimu sana kuzuia utuamishaji wa maji na mlipuko wa magojwa ya miche. Pia inashauriwa kung’oa magugu na uvunaji ufanywe kwa  mkono.

MATUMIZI YA MBOLEA
Vitunguu hufanya vizuri kama shamba litawekewa mbolea ya samadi au mboji iliyoiva vizuri. Kiasi cha tani 25-40 kwa heka kinashauriwa. Hii ni sawa na kilo7.5 -12 kwa tuta lenye urefu wa mita 3 na upana wa mita 1.



UMUHIMU WA PALIZI KWENYE VITUNGUU.
Palizi kwenye zao la vitunguu ni muhimu sana kwa sababu ya kuongeza kipato. Kwani magugu yanauwezo wa Mkubwa mno wa kuchukua virutubisho vingi kwenye ardhi kuliko vitunguu, hivyo hupelekea vitunguu kupunguza uzaaji nzuri na kusababisha upungufu wa mavuno kutokea. Magugu hayo yanaweza kudhibitiwa kupitia jembe la mkono, ung'oaji magugu kwa kutumia mkono, au kutumia madawa ya kuja wadudu.
MAGONJWA YA VITUNGUU MAJI
Kuna magonjwa mbalimbali yanayosumbua zao la kitunguu, lakini magonjwa makubwa yanayojitokeza sana katika ZAO hili ni pamoja na ;
1.      Ukungu wa unga (powdery mildew) na wa chini (downy mildew).
Magonjwa haya hushambulia majani ya mimea shambani na hata miche michanga. Katika majani huonekana vidoa vyeupe hasa kwenye majani makuu ya mimea michanga. Kwani ugonjwa huu hutokea na kuongezeka kwa haraka kwenye sehemu za baridi au nyakati za baridi. Ugonjwa juu unaweza kudhibitiwa na dawa kama mancozeb.
2.      Ugonjwa wa doa la pinki (Purple blotch)
Ugonjwa huu huanza kama doa dogo linalozama ndani ya nani na kisha linaongezeka ukubwa na kufanya ranging ya pinki. Kiini cha ugonjwa juu huanzia kwenye mbegu na pia hubakia kwenye maozo ya majani ya vitunguu.
Udhibiti wa ugonjwa juu ni kulima Kilimo cha kubadilisha mazao (crop rotation). Pia tunaweza kudhibiti ugonjwa huu kwa kuzuia kutuama kwa maji shambani, msongamano wa mazao shambani na matumizi ya mbolea zenye calcium, phosphate na potassium hupunguza kuenea kwa ugonjwa juu.


3.      Kuoza kwa vitunguu (bulb rots)
Ugonjwa juu ni hatari zaidi huweza kutoka shambani au wakati wa hifadhi ghalani. Ugonjwa juu huweza kujitokeza zaidi sehemu zenye joto na kutuamisha maji.
Udhibiti wake kuhakikisha shambani hakuna hali ya kutuamisha maji na pia kwenye ghala kuna kuwa na hali nzuri ya mzunguko wa hewani.
WADUDU WANAOSHAMBULIA ZAO LA KITUNGUU.
Kati ya wadudu wasumbufu wa zao la kitunguu ni pamoja na ;
1.      Utitiri wa vitunguu (Onion thrips)
Hawa ni wadudu wadogowadogo sana ambao hula kwa kukwaruza juu ya jani na kunyonya majimaji ya kwenye mmea. Hali ambayo hupelekea kutoka kwa mikwaruzo meupe kwenye majani ya vitunguu, hali ambayo ikizidi hupelekea kunyauka kwa majani ya mmea na hatimaye majani hayo kuanguka, vile vile husababisha kupungua kwa ukubwa wa vitunguu. Tatizo la hao wadudu hujitokeza zaidi nyakati za ukame kuliko wakati wa unyevu.
2.      Bungua weupe (white grub)
Huyu ni aina ya funza Mkubwa hutaga mayai yake kwenye uozo wa majani na samadi, hivyo mashamba ya vitunguu ambayo hapo kwenye maeneo hayo au karibu na maeneo ya jinsi hiyo yapo kwenye hatari kubwa zaidi ya kukabiliwa na tatizo hilo la hao wadudu.
Kwa wadudu hao hushambulia mizizi ya mmea wa kitunguu na kusababisha mmea huo unyauke, na hatimaye hufa. Wadudu hao tunaweza kuwa punguza kwa kutifulia shamba na kuwaweka wazi wadudu 




UVUNAJI
Vitunguu huvunwa kuanzia siku 90-150 tangu kusia mbegu. Dalili za kukomaa ni kuanguka kwa majani. Vitunguu huvunwa kwa kuvuta kwa mkono na kuhifadhiwa siku kadhaa shambani vikiwa vimefunikwa na majani. Baada ya hapo majani hukatwa na balbu hupakiwa kwa ajili ya kuhifadhi kusubiria bei nzuri. Vitunguu huweza kuhifadhiwa hadi miezi 9 tangu vivunwe bila kuharibika. Vitunguu vihifadhiwe kwenye nyuzi joto chini ya 4.4 °C ama juu ya nyuzijoto 25°C ili visiharibike.

UUZAJI
Vitunguu ni zao lenye bei nzuri ukilinganisha na mazao mengine ya mbogamboga na huuzwa kwenye masoko ya kawaida kwa bei nzuri.
Kama vitunguu vikilimwa vizuri na kuhudumiwa ipasavyo Ekari moja huzaa gunia 70-90 sawa na kg 7000-9000. Kama akipata soko la uhakika mkulima anaweza kupata hadi 13.5 milioni kwa msimu mmoja

UMUHIMU WA ZAO LA KITUNGUU
1. Kuongea kipato cha mkulima
2. Chanzo cha ajira
3. Huongeza pato la Taifa na kuchangia katika maendeleo ya Taifa
4. Hutumika kama mboga na kiungo

For more info:

No comments:

Post a Comment

Habari zilizopita

KILIMO CHA KOROSHO

KILIMO CHA KOROSHO UTANGULIZI Korosho ni zao la biashara ambalo chimbuko lake ni Ureno na baadae mnamo karne ya 16 ndipo li...