Friday, June 27, 2025

KILIMO BORA CHA MALIMAO


Limao ni tunda jamii ya Citrus lenye ladha ya kipekee, utajiri wa vitamini C, na linatumika sehemu mbali mbali, mfano kwenye mapishi, vinywaji, na dawa za asili. Zao hili hustawi vizuri sana katika maeneo yenye hali ya hewa ya joto. Limao linaweza kulimwa kwa ajili ya matumizi ya nyumbani na kibiashara, ni zao lenye faida kubwa kiuchumi kwa wakulima wa Tanzania.

Makala hii ni muongozo wa kina kuhusu kilimo bora cha limao, kuanzia hali ya hewa inayofaa, aina ya udongo, mbinu za upandaji, matunzo ya shamba, hadi mavuno.

1. Hali ya Hewa na Udongo Unaofaa kwa Kilimo cha Limao

1.1. Hali ya Hewa

Limao hustawi vizuri katika maeneo yenye hali ya hewa ya joto la wastani hadi joto kali.

Wastani wa joto bora kwa kilimo cha limao ni kati ya nyuzi joto 25°C hadi 30°C.

Limao linahitaji mvua kati ya milimita 1000 hadi 1500 kwa mwaka ili kustawi vizuri.

Hata hivyo, linavumilia pia vipindi vya ukame, mradi umwagiliaji ufanyike wakati wa ukame mkali.

1.2. Udongo.

Limao hustawi kwenye udongo wenye rutuba ya wastani, unaopitisha maji kwa urahisi.

Udongo wa mchanganyiko wa mchanga na tifutifu au mchanga wa asili unafaa zaidi kwa kilimo cha limao.

Udongo wa mfinyanzi mzito haupendekezwi kwa sababu unashikilia maji mengi, jambo ambalo linaweza kusababisha kuoza kwa mizizi.

Limao hustawi vizuri kwenye udongo wenye pH kati ya 5.5 hadi 6.5.

2. Maandalizi ya Shamba kwa Kilimo cha Limao

2.1. Kuchagua Eneo

Eneo la kulima limao linapaswa kuwa na mwanga wa kutosha, kwa sababu limao linahitaji mwanga wa jua kwa angalau masaa 6 hadi 8 kila siku.

Pia, eneo linapaswa kuwa na mifereji mizuri ya maji ili kuzuia maji kutuama kwenye udongo.

2.2. Kuandaa Udongo

Shamba linapaswa kulimwa vizuri na kusafishwa magugu na vichaka vyote.

Ni muhimu kuhakikisha kuwa udongo unakokotolewa kwa kutumia jembe au trekta ili kuruhusu mizizi ya mimea kupenyeza kwa urahisi.

Kabla ya kupanda, ni vyema kuongeza mbolea ya samadi au mboji ili kuboresha rutuba ya udongo.

3. Uchaguzi wa Mbegu na Upandaji wa Limao

3.1. Uchaguzi wa Mbegu

Limao linaweza kuzalishwa kwa kutumia mbegu au kwa kutumia vipandikizi(Grafted).

Mbegu kawaida huchukua muda mrefu kuchipua na kuzaa matunda, hivyo vipandikizi ni bora zaidi kwa kilimo cha kibiashara.

Vipandikizi huchukuliwa kutoka kwa miti yenye afya, na lazima viwe vimekomaa na kuchaguliwa kwa uangalifu ili kupata mimea yenye ubora.

3.2. Upandaji wa Limao

Miche ya limao inapandwa shambani ikiwa na umri wa miezi 6 hadi 12.

Nafasi ya kupanda inapaswa kuwa mita 6 x 6 au 7×7 kati ya mche mmoja na mwingine ili kuruhusu mimea kukua vizuri bila kuathiriana.

Mashimo yenye urefu na upana wa sentimeta 60 yanapaswa kuchimbwa, na kujazwa mbolea ya samadi au mboji kabla ya kupanda mche.

Ni vyema kupanda limao mwanzoni mwa msimu wa mvua ili mimea ipate maji ya kutosha katika hatua za mwanzo za ukuaji.

4. Matunzo ya Shamba la Limao

4.1. Umwagiliaji

Ingawa limao linaweza kuvumilia vipindi vya ukame, umwagiliaji wa mara kwa mara unahitajika hasa wakati wa ukame.

Umwagiliaji mara mbili au tatu kwa wiki ni muhimu katika miezi ya kwanza baada ya kupanda ili kuwezesha mizizi kujikita vizuri.

Baada ya miti kukomaa, unaweza kupunguza umwagiliaji lakini ni muhimu kuhakikisha kuwa miti inapata unyevu wa kutosha.

4.2. Mbolea

Mbolea za asili kama samadi au mboji ni muhimu katika hatua za mwanzo za ukuaji wa mimea.

Mbolea za viwandani kama NPK zinaweza kutumika kila baada ya miezi mitatu ili kuimarisha ukuaji wa mimea na kuleta mazao bora.

Wakulima wanashauriwa kutumia mbolea ya fosfeti kusaidia ukuaji mzuri wa mizizi.

4.3. Palizi

Palizi ya mara kwa mara ni muhimu ili kuondoa magugu ambayo yanaweza kushindana na mimea kwa virutubisho na maji.

Palizi inapaswa kufanyika kwa uangalifu ili kuepuka kuharibu mizizi ya miti ya limao, hasa katika hatua za mwanzo za ukuaji.

4.4. Kupogoa

Kupogoa ni hatua muhimu kwa kilimo cha limao ili kuzuia matawi yasiyo na tija na kusaidia mzunguko mzuri wa hewa.

Matawi yaliyozeeka, magonjwa, au yasiyo na tija yanapaswa kupogolewa mara kwa mara ili kuruhusu matawi mapya kukua vizuri na kuzaa matunda bora.

4.5. Udhibiti wa Wadudu na Magonjwa

Limao linaweza kushambuliwa na wadudu kama vile minyoo, vidukari, na buibui wekundu.

Pia, magonjwa kama vile ugonjwa wa madoa ya majani na kuoza kwa mizizi yanaweza kuathiri mimea.

Ni muhimu kutumia viuatilifu vinavyoshauriwa na wataalamu wa kilimo ili kudhibiti wadudu na magonjwa.

Mimea inapaswa kufuatiliwa mara kwa mara ili kubaini matatizo mapema na kuyadhibiti.

5. Mavuno ya Limao

Limao linaanza kutoa matunda baada ya miaka 2 hadi 3 tangu kupandwa, kutegemea na aina ya mche na matunzo.

Mavuno hufanyika mara moja au mbili kwa mwaka, kutegemea hali ya hewa na eneo. Limao huvunwa pale yanapobadilika rangi kuwa ya kijani kibichi au kijani kikavu.

Matunda yanapaswa kuvunwa kwa uangalifu ili yasiharibiwe na pia kuhakikisha kuwa yanakidhi viwango vya soko.

Baada ya kuvuna, limao linaweza kuhifadhiwa kwenye mazingira ya baridi ili kuongeza muda wa matumizi bila kuharibika.

6. Masoko ya Limao

6.1. Soko la Ndani

Limao lina soko kubwa la ndani kutokana na matumizi yake mengi kwenye vinywaji, vyakula, na bidhaa za vipodozi.

Matunda haya yanaweza kuuzwa moja kwa moja kwenye masoko ya wazi, maduka ya vyakula, au kwa wafanyabiashara wa jumla.

Pia, kuna viwanda vidogo na vikubwa ambavyo vinatengeneza bidhaa kama vile juisi ya limao na bidhaa za urembo, hivyo kuongeza fursa ya soko.

6.2. Soko la Nje

Tanzania inaweza kusafirisha limao kwenye masoko ya kimataifa, hasa kwa nchi jirani na zingine za Afrika na Mashariki ya Kati.

Ili kuuza limao kwenye soko la kimataifa, ni muhimu kuhakikisha kuwa matunda yanakidhi viwango vya ubora vya kimataifa.

Limao lazima lichambuliwe vizuri na lifungwe kwa usafi ili kuepusha kuharibika wakati wa usafirishaji.

Hitimisho

Kilimo cha limao ni fursa nzuri kwa wakulima kutengeneza kipato cha kudumu kutokana na soko lake la ndani na nje.

Kwa kufuata mbinu bora za kilimo, wakulima wanaweza kupata mavuno mengi na yenye ubora.

  Paul F. Kisena.                                                        BSc. Agricultural Economics.                                      Sokoine university of Agriculture.                              Phone: +255683937375/+255713014501


Tuesday, October 30, 2018

KILIMO CHA KOROSHO


KILIMO CHA KOROSHO




UTANGULIZI
Korosho ni zao la biashara ambalo chimbuko lake ni Ureno na baadae mnamo karne ya 16 ndipo lilipofika Afrika, katika nchi ya mozamboque na baadae likafika Kenya na Tanzania.
Tanzania zao la korosho ulimwa na kustawi vizuri katika pwani yote ya bahari ya Hindi Kuanzia Mtwara Mpaka Tanga, pia ipo mikoa mipya kamaTABORA,SINGIDA,DODOMA,SOGWE,RUKWA huko kote zao la korosho linastawi vizuri
Mvua na Udongo

Korosho hustawi vizuri kwenye maeneo yenye mvua 840mm - 1250 mm wastani wa mvua kwa mwaka, napia hukua vizuri kwenye maeneo 0- 500 m kutoka usawa wa bahari.

Kutokana na kwamba samadi sehemu nyingi ni adimu, mbolea za viwandani zinafaa kutumika katika kupandia, husaidia kukuza haraka japo ukipanda bila mbolea miti inaota na utavuna kama kawaida ila tofauti ya kutumia mbolea husaidia kukua kwa haraka.
Mikorosho haihitaji maji kilasiku ukuaji hautakuwa mzuri ,kwa kipindi cha kiangazi umwagiliaji mzuri ni ndoo ya lita kumi kwa kila shimo kwa wiki moja inatosha sana,ila kama utakuwa una miche iliyofikia upana wa peni na ukapanda kipindi cha mvua na mche ukapata mvua kwa miezi 4-5 inatosha sana kuendelea kukua wenyewe.
Pia kama ni kipindi cha kiangazi unaweza kuzungushia mche na majani makavu kwa kuhifadhi unyevu.
Korosho hukua vizuri kwenye maeneo yenye PH 5.6 udongo wa kichanga (sandy) na pia udongo mfinyazi kichanga.

MAANDALIZI YA SHAMBA
Korosho kama mazao mengine shamba linatakiwa kusafishwa, kusawazishwa nakutifuliwa vizuri kwaajili ya kupanda korosho.
Katika mashimo utakayo chimba unaweza kuweka mbolea ya ngombe ukachanganya na udongo mapema ili kuongeza rutuba.








JINSI YA KUPANDA
Ni muhimu sana   kuchagua mbegu bora kwakua mbegu utakayoipanda ndio itakuonyesha kiasi gani utavuna,
Baada ya kununua mbegu unachukua maji na chumvi 100g ya chumvi unaweka katika maji kiasi cha lita 5 unakoroga vizuri na unachukua mbegu zako unaweka kwenye maji hayo zile zitakazo zama ndio mbegu zenye uwezekano mkubwa wa kiota,
Kitaalamu hekari moja inatakiwa ichukue miche 25-27 ambapo ni space ya mita 12 urefu na 12 upana kwa mbegu za kienyeji
Kwa kilimo cha kisasa nikimaanisha mbegu bora za kisasa na kwa mpango wa upandaji bila kuchanganya na mazao mengine hekari moja inakaa mpaka miti 100 na mkorosho uliostawi vizuri unatoa kuanzia kilo 10-20.Kwa hiyo unauhakika wa kuvuna kuanzia tani moja ya korosho kila heka ambayao tani moja sio chini ya milioni 3
Mikorosho ile ya kubebesha ya muda mfupi inaanza kutoa Korosho kuanzia miaka mitatu, Huwa wanasema miaka miwili au mmoja ni kweli ila unakuwa hauna nguvu, unashauriwa kutoa mau yote ili uweze kutengeneza matawi na kuwa na nguvu.

AINA ZA UPANDAJI MBEGU
Kupanda moja kwa moja
Hii ni njia mambayo ni hatarishi sana na inaitaji umakini kwa sababu  kuna uwezekano mkubwa wa mbegu kufa. ukitumia njia hii unatakiwa kupanda mbegu tatu 3 katika shimo moja na baada ya miezi mi 3 - 4 ng’oa mimea na bakiza mmoja wenye afya na muonekano mzuri.
Njia ya kitaru
Hii ni njia ya pili na ni nzuri kwa sababu unakua huru kuchagua mche ambao umestawi na ulio na muonekano mzuri , unatakiwa kuamishia miche shambani ikiwa na umri wa wiki 6 na zingatia kuchagua mche wenye afya na baadae unatakiwa kupunguza majani urefu wa sm60- 90 kutoka kwenye ardhi na pia ondoa majani yote ambayo yanaonekana kuadhiliwa na magonjwa au wadudu.
MAGONJWA NA WADUDU

MAGONJWA
  • Anthracnose
  • Powdery mildew
Hayo ni baadhi ya magonjwa yanayo athiri sana korosho

WADUDU
  • Cashew stem girdler
  • Cashew weevil
  • coconut bug
  • heliotropes bug
 KUZUIA NA TIBA
Ili kuweza kuzuia maagonjwa na wadudu unatakiwa kuzingatia yafuatayo: 
  • Palilia mapema
  • Weka shamba katika hali ya usafi
  • Tumia mbinu ya kuchanganya mazao kwa korosho unaweza kuchanya pamba au maharagwe hiyo inasaidia kukimbiza wadudu wengine ambao wanakua hawapatani na mazao hayo
  • Tumia pesticide kutibu magonjwa na insecticide kuuwa wadudu wahalibifu

Uwekezaji
Wengi wananua mashamba yenye mikorosho then wanaindeleza kwa kupanda niche mipya,ambapo ikianza kuzaa kwa wingi ndipo hukata ya zamani.Ila kipindi hiki kuuziwa shamba LA mikorosho ni shughuli cze in sawa na kuuza kitalu cha madini.





PAUL FABIAN KISENA
BSc. Agricultural Economics and Agribusiness
Sokoine University of Agriculture
Cont: 0683937375/0713014501
Email: kisenapaul@gmail.com

Monday, September 10, 2018

UFUGAJI WA SAMAKI




UTANGULIZI
Ufugaji wa samaki unakua kwa kasi sana hapa nchini tanzania kutokana na kuonekana kua na faida sana. hivyo nimeamua leo nikupe elimu kidogo ambayo itakusaidia wewe mfugaji ambaye ungependa kujikita katika ufugaji huo, hivyo tue pamoja ili kujua mengi.
Kuna aina nyingi za samaki wa maji baridi ambao wanaweza kufugika kwa urahisi au ugumu kidogo tu na aina hizo wapo wale ambao sio wa kuzaliana(monosexual) na wale wa kuzaliana(heterosexual)
Wapo samaki aina ya Sato(Tilapia),Kambale(African catfish) na wengine aina ya pangasius ambao hufugwa kwa wingi sana.
Urahisi hapa uko zaidi kwenye kuwafuga wasiozaliana sababu hawaongezeki wakati wale wanaozaliana utakuwa na utaratibu wa kuhamisha fishling(vifaranga) sehemu nyingine.
 

UTENGENEZAJI WA BWAWA
Kuna aina mbali mbali za kutengeneza mabwawa ya samaki inategemea na eneo, kiasi cha samaki unao taka kufuga, aina ya samaki na hali ya uchumi.
Rasilimali muhimu za kuwa nazo ili kufanikisha shughuli hii ni eneo la ardhi,maji, rasilimali watu na rasilimali fedha. 

Eneo la ardhi ndio litakaloonyesha ni kwa namna gani bwawa lako liwe,aidha la kujengea na cement,kutandika plastic au kuchimba na kulitumia hivyohivyo.Bwawa huchimbwa/kujengwa kwa kuwa na sakafu yenye ulalo kiasi(gentle slope/gradient)
Unahitaji samaki 7-8 katika meter moja ya mraba(1m^2) ,kwa maana hiyo kama una meter za mraba 600 nasi unaweza kufuga samaki 4500.Haishauriwi kulundika samaki kwenye eneo dogo kwani itawasababishia ukosefu wa hewa(oxygen).Ingawa zipo njia za kuweza kuongeza upatikanaji wa hewa kwenye mabwawa.

Ukishachimba bwawa lako(aidha na kulijengea) unaingiza maji kwenye bwawa hakikisha yamekaribia futi 2.5 mpaka kujaa full.Itakubidi kufanya liming(kumwagia chokaa bwawa kabla ya kuweka maji ili kuua bacteria hatarishi kwa maisha na afya ya samaki wako) pia unahitajika kuyarutubisha hayo maji kwa kuchanganya na mbolea(kama ya ng’ombe na za viwandani pia ingawa haishauriwi sana) na kusubiria kwa muda usiopungua siku 21 au zaidi.Unafanya hivi ili kuweka mazingira ya chakula asili(natural foood) kwa ajili ya samaki kujitengeneza,vyakula hivo hua katika hali ya mimea na viumbe wadogo(microorganisms)

Upatikanaji wa vifaranga vya samaki,hapa inakubidi uwe makini sana kama umeamua kuzalisha sato,changamoto kubwa ya sato ni kupata mbegu ambayo under right conditions vifaranga vitaweza kua samaki wenye uzito wa kutosha(miezi 6 awe at least 500grams au zaidi).Mbegu ya sato hupatikana kwa bei rejareja ya sh 300 na kambale sh 500 kwa kifaranga kimoja.Wapo wazalishaji wengi wa mbegu za vifaranga wa ndani na nje ya nchi ila kwa Tanzania nimewakubali Tanzania Fisheries Research Institute(TAFIRI) Nyegezi,Mwanza
Ulishaji wa vifaranga vyako ,chakula chao kinategemea na uzito wao mfano samaki hula 5% ya uzito wake wa mwili akiwa mdogo na 3% akiwa mkubwa.Hapa tunaongelea ulishaji wa chakula cha ziada(supplement food),sababu cha asili amekipata kwenye ile mbolea ulioweka.Kama una vifaranga 100 vyenye gram 10 kila kimoja basi utahitaji gram 50 kuwalisha.
Itakuchukua Miezi 6-9 kuanza kuvuna samaki wako ambao unaweza kuwauza kulingana na uzito au au njia utayoona inakufaa.Samaki wengi wa kwenye mabwawa wanavunwa kwa kutumia nyavu au kumwaga maji yote nje ya bwawa.Masoko yake haya samaki ni pamoja na supermarkets, wafanyabiashara sokoni na mitaani pamoja na watu binafsi.

UPANDIKIZAJI WA VIFARANGA/MBEGU ZA SAMAKI KATIKA BWAWA
Kabla vifaranga hawaja safirishwa ni vyema kuwatoa katika bwa kubwa wanalo ishi na kuwaweka katika vibwa vidogo vidogo  kati ya masaa 24 hadi 72 kuendana na umbali wa safari bila kuwapa chakula chochote kile.
  • baada ya kuwasafirisha mfugaji  atakiwi kuviweka kwenye bwa moja kwa moja ila inatakiwa maji yalio tumika katika kuwasafirisha yabadilishane joto na maji ya bwawa ambalo wataenda kuishi. hivyo mfugaji anatakiwa kuliweka kontena ambalo vifaranga wamo ndani ya bwawa ambalo wataishi kwa dakika 30 hadi 35 bila kuwafungulia, baada ya hapo kontena liina mishwe taratibu ili kuwezesha maji ya bwawa na yaliyo kwenye kontena kubadilishana na baadae vifaranga watatoka taratibu,
endapo hautafanya hivyo  unaweza kusababisha vifaranga vyote kufa kutokana na mabadiliko   ya joto ambayo yanaweza kutokea ghafla.
  • unatakiwa kusafirisha vifaranga wako mda ambao hali ya hewa inakua sio joto yaan mda wa jion na asubuhi ili kuwezesha vifaranga kuimili misukosuko ya safari na bila kupatwa na joto kali.
CHAKULA NA UTUNZAJI WA SAMAKI BWAWANI
  • Samaki hutakiwa kupewa chakula angalau mara 2 kila  siku  unatakiwa kuzingatia mda sahihi wa kuwapa chakula yaan asubuhi saa 3-4 na jion saa 9 -10 samaki upewa vyakula tofauti kulingana na aina. 
Tabia ya ulaji wa samaki
  1. samaki wanao kula nyama (sangara, kambale)
  2. samaki wanao kula mimea carps
  3. samaki wanao kula mchanganyiko (perege,sato na samaki wa maji ya chumvi mfano kibua)


TARATIBU ZA ULISHAJI WA SAMAKI

UMRI(wiki)

UZITO(gm)

KIASI CHA CHAKULA KWA SIKU (gm)
1-2
5-10
1
2-3
20-50
2
3-5
50-110
3
5-7
110-200
4
7 nakuendelea

200 na zaidi

5



kaluluagribusiness@gmail.com
Intagram: KALULUAGRIBUSINESS
Facebookpage: KALULU AGRIBUSINESS SOLUTIONS
0713014501 /0683937375

                                                

Habari zilizopita

KILIMO BORA CHA MALIMAO

Limao ni tunda jamii ya Citrus lenye ladha ya kipekee, utajiri wa vitamini C, na linatumika sehemu mbali mbali, mfano kwenye mapishi, vinywa...