Tuesday, October 30, 2018

KILIMO CHA KOROSHO


KILIMO CHA KOROSHO




UTANGULIZI
Korosho ni zao la biashara ambalo chimbuko lake ni Ureno na baadae mnamo karne ya 16 ndipo lilipofika Afrika, katika nchi ya mozamboque na baadae likafika Kenya na Tanzania.
Tanzania zao la korosho ulimwa na kustawi vizuri katika pwani yote ya bahari ya Hindi Kuanzia Mtwara Mpaka Tanga, pia ipo mikoa mipya kamaTABORA,SINGIDA,DODOMA,SOGWE,RUKWA huko kote zao la korosho linastawi vizuri
Mvua na Udongo

Korosho hustawi vizuri kwenye maeneo yenye mvua 840mm - 1250 mm wastani wa mvua kwa mwaka, napia hukua vizuri kwenye maeneo 0- 500 m kutoka usawa wa bahari.

Kutokana na kwamba samadi sehemu nyingi ni adimu, mbolea za viwandani zinafaa kutumika katika kupandia, husaidia kukuza haraka japo ukipanda bila mbolea miti inaota na utavuna kama kawaida ila tofauti ya kutumia mbolea husaidia kukua kwa haraka.
Mikorosho haihitaji maji kilasiku ukuaji hautakuwa mzuri ,kwa kipindi cha kiangazi umwagiliaji mzuri ni ndoo ya lita kumi kwa kila shimo kwa wiki moja inatosha sana,ila kama utakuwa una miche iliyofikia upana wa peni na ukapanda kipindi cha mvua na mche ukapata mvua kwa miezi 4-5 inatosha sana kuendelea kukua wenyewe.
Pia kama ni kipindi cha kiangazi unaweza kuzungushia mche na majani makavu kwa kuhifadhi unyevu.
Korosho hukua vizuri kwenye maeneo yenye PH 5.6 udongo wa kichanga (sandy) na pia udongo mfinyazi kichanga.

MAANDALIZI YA SHAMBA
Korosho kama mazao mengine shamba linatakiwa kusafishwa, kusawazishwa nakutifuliwa vizuri kwaajili ya kupanda korosho.
Katika mashimo utakayo chimba unaweza kuweka mbolea ya ngombe ukachanganya na udongo mapema ili kuongeza rutuba.








JINSI YA KUPANDA
Ni muhimu sana   kuchagua mbegu bora kwakua mbegu utakayoipanda ndio itakuonyesha kiasi gani utavuna,
Baada ya kununua mbegu unachukua maji na chumvi 100g ya chumvi unaweka katika maji kiasi cha lita 5 unakoroga vizuri na unachukua mbegu zako unaweka kwenye maji hayo zile zitakazo zama ndio mbegu zenye uwezekano mkubwa wa kiota,
Kitaalamu hekari moja inatakiwa ichukue miche 25-27 ambapo ni space ya mita 12 urefu na 12 upana kwa mbegu za kienyeji
Kwa kilimo cha kisasa nikimaanisha mbegu bora za kisasa na kwa mpango wa upandaji bila kuchanganya na mazao mengine hekari moja inakaa mpaka miti 100 na mkorosho uliostawi vizuri unatoa kuanzia kilo 10-20.Kwa hiyo unauhakika wa kuvuna kuanzia tani moja ya korosho kila heka ambayao tani moja sio chini ya milioni 3
Mikorosho ile ya kubebesha ya muda mfupi inaanza kutoa Korosho kuanzia miaka mitatu, Huwa wanasema miaka miwili au mmoja ni kweli ila unakuwa hauna nguvu, unashauriwa kutoa mau yote ili uweze kutengeneza matawi na kuwa na nguvu.

AINA ZA UPANDAJI MBEGU
Kupanda moja kwa moja
Hii ni njia mambayo ni hatarishi sana na inaitaji umakini kwa sababu  kuna uwezekano mkubwa wa mbegu kufa. ukitumia njia hii unatakiwa kupanda mbegu tatu 3 katika shimo moja na baada ya miezi mi 3 - 4 ng’oa mimea na bakiza mmoja wenye afya na muonekano mzuri.
Njia ya kitaru
Hii ni njia ya pili na ni nzuri kwa sababu unakua huru kuchagua mche ambao umestawi na ulio na muonekano mzuri , unatakiwa kuamishia miche shambani ikiwa na umri wa wiki 6 na zingatia kuchagua mche wenye afya na baadae unatakiwa kupunguza majani urefu wa sm60- 90 kutoka kwenye ardhi na pia ondoa majani yote ambayo yanaonekana kuadhiliwa na magonjwa au wadudu.
MAGONJWA NA WADUDU

MAGONJWA
  • Anthracnose
  • Powdery mildew
Hayo ni baadhi ya magonjwa yanayo athiri sana korosho

WADUDU
  • Cashew stem girdler
  • Cashew weevil
  • coconut bug
  • heliotropes bug
 KUZUIA NA TIBA
Ili kuweza kuzuia maagonjwa na wadudu unatakiwa kuzingatia yafuatayo: 
  • Palilia mapema
  • Weka shamba katika hali ya usafi
  • Tumia mbinu ya kuchanganya mazao kwa korosho unaweza kuchanya pamba au maharagwe hiyo inasaidia kukimbiza wadudu wengine ambao wanakua hawapatani na mazao hayo
  • Tumia pesticide kutibu magonjwa na insecticide kuuwa wadudu wahalibifu

Uwekezaji
Wengi wananua mashamba yenye mikorosho then wanaindeleza kwa kupanda niche mipya,ambapo ikianza kuzaa kwa wingi ndipo hukata ya zamani.Ila kipindi hiki kuuziwa shamba LA mikorosho ni shughuli cze in sawa na kuuza kitalu cha madini.





PAUL FABIAN KISENA
BSc. Agricultural Economics and Agribusiness
Sokoine University of Agriculture
Cont: 0683937375/0713014501
Email: kisenapaul@gmail.com

Monday, September 10, 2018

UFUGAJI WA SAMAKI




UTANGULIZI
Ufugaji wa samaki unakua kwa kasi sana hapa nchini tanzania kutokana na kuonekana kua na faida sana. hivyo nimeamua leo nikupe elimu kidogo ambayo itakusaidia wewe mfugaji ambaye ungependa kujikita katika ufugaji huo, hivyo tue pamoja ili kujua mengi.
Kuna aina nyingi za samaki wa maji baridi ambao wanaweza kufugika kwa urahisi au ugumu kidogo tu na aina hizo wapo wale ambao sio wa kuzaliana(monosexual) na wale wa kuzaliana(heterosexual)
Wapo samaki aina ya Sato(Tilapia),Kambale(African catfish) na wengine aina ya pangasius ambao hufugwa kwa wingi sana.
Urahisi hapa uko zaidi kwenye kuwafuga wasiozaliana sababu hawaongezeki wakati wale wanaozaliana utakuwa na utaratibu wa kuhamisha fishling(vifaranga) sehemu nyingine.
 

UTENGENEZAJI WA BWAWA
Kuna aina mbali mbali za kutengeneza mabwawa ya samaki inategemea na eneo, kiasi cha samaki unao taka kufuga, aina ya samaki na hali ya uchumi.
Rasilimali muhimu za kuwa nazo ili kufanikisha shughuli hii ni eneo la ardhi,maji, rasilimali watu na rasilimali fedha. 

Eneo la ardhi ndio litakaloonyesha ni kwa namna gani bwawa lako liwe,aidha la kujengea na cement,kutandika plastic au kuchimba na kulitumia hivyohivyo.Bwawa huchimbwa/kujengwa kwa kuwa na sakafu yenye ulalo kiasi(gentle slope/gradient)
Unahitaji samaki 7-8 katika meter moja ya mraba(1m^2) ,kwa maana hiyo kama una meter za mraba 600 nasi unaweza kufuga samaki 4500.Haishauriwi kulundika samaki kwenye eneo dogo kwani itawasababishia ukosefu wa hewa(oxygen).Ingawa zipo njia za kuweza kuongeza upatikanaji wa hewa kwenye mabwawa.

Ukishachimba bwawa lako(aidha na kulijengea) unaingiza maji kwenye bwawa hakikisha yamekaribia futi 2.5 mpaka kujaa full.Itakubidi kufanya liming(kumwagia chokaa bwawa kabla ya kuweka maji ili kuua bacteria hatarishi kwa maisha na afya ya samaki wako) pia unahitajika kuyarutubisha hayo maji kwa kuchanganya na mbolea(kama ya ng’ombe na za viwandani pia ingawa haishauriwi sana) na kusubiria kwa muda usiopungua siku 21 au zaidi.Unafanya hivi ili kuweka mazingira ya chakula asili(natural foood) kwa ajili ya samaki kujitengeneza,vyakula hivo hua katika hali ya mimea na viumbe wadogo(microorganisms)

Upatikanaji wa vifaranga vya samaki,hapa inakubidi uwe makini sana kama umeamua kuzalisha sato,changamoto kubwa ya sato ni kupata mbegu ambayo under right conditions vifaranga vitaweza kua samaki wenye uzito wa kutosha(miezi 6 awe at least 500grams au zaidi).Mbegu ya sato hupatikana kwa bei rejareja ya sh 300 na kambale sh 500 kwa kifaranga kimoja.Wapo wazalishaji wengi wa mbegu za vifaranga wa ndani na nje ya nchi ila kwa Tanzania nimewakubali Tanzania Fisheries Research Institute(TAFIRI) Nyegezi,Mwanza
Ulishaji wa vifaranga vyako ,chakula chao kinategemea na uzito wao mfano samaki hula 5% ya uzito wake wa mwili akiwa mdogo na 3% akiwa mkubwa.Hapa tunaongelea ulishaji wa chakula cha ziada(supplement food),sababu cha asili amekipata kwenye ile mbolea ulioweka.Kama una vifaranga 100 vyenye gram 10 kila kimoja basi utahitaji gram 50 kuwalisha.
Itakuchukua Miezi 6-9 kuanza kuvuna samaki wako ambao unaweza kuwauza kulingana na uzito au au njia utayoona inakufaa.Samaki wengi wa kwenye mabwawa wanavunwa kwa kutumia nyavu au kumwaga maji yote nje ya bwawa.Masoko yake haya samaki ni pamoja na supermarkets, wafanyabiashara sokoni na mitaani pamoja na watu binafsi.

UPANDIKIZAJI WA VIFARANGA/MBEGU ZA SAMAKI KATIKA BWAWA
Kabla vifaranga hawaja safirishwa ni vyema kuwatoa katika bwa kubwa wanalo ishi na kuwaweka katika vibwa vidogo vidogo  kati ya masaa 24 hadi 72 kuendana na umbali wa safari bila kuwapa chakula chochote kile.
  • baada ya kuwasafirisha mfugaji  atakiwi kuviweka kwenye bwa moja kwa moja ila inatakiwa maji yalio tumika katika kuwasafirisha yabadilishane joto na maji ya bwawa ambalo wataenda kuishi. hivyo mfugaji anatakiwa kuliweka kontena ambalo vifaranga wamo ndani ya bwawa ambalo wataishi kwa dakika 30 hadi 35 bila kuwafungulia, baada ya hapo kontena liina mishwe taratibu ili kuwezesha maji ya bwawa na yaliyo kwenye kontena kubadilishana na baadae vifaranga watatoka taratibu,
endapo hautafanya hivyo  unaweza kusababisha vifaranga vyote kufa kutokana na mabadiliko   ya joto ambayo yanaweza kutokea ghafla.
  • unatakiwa kusafirisha vifaranga wako mda ambao hali ya hewa inakua sio joto yaan mda wa jion na asubuhi ili kuwezesha vifaranga kuimili misukosuko ya safari na bila kupatwa na joto kali.
CHAKULA NA UTUNZAJI WA SAMAKI BWAWANI
  • Samaki hutakiwa kupewa chakula angalau mara 2 kila  siku  unatakiwa kuzingatia mda sahihi wa kuwapa chakula yaan asubuhi saa 3-4 na jion saa 9 -10 samaki upewa vyakula tofauti kulingana na aina. 
Tabia ya ulaji wa samaki
  1. samaki wanao kula nyama (sangara, kambale)
  2. samaki wanao kula mimea carps
  3. samaki wanao kula mchanganyiko (perege,sato na samaki wa maji ya chumvi mfano kibua)


TARATIBU ZA ULISHAJI WA SAMAKI

UMRI(wiki)

UZITO(gm)

KIASI CHA CHAKULA KWA SIKU (gm)
1-2
5-10
1
2-3
20-50
2
3-5
50-110
3
5-7
110-200
4
7 nakuendelea

200 na zaidi

5



kaluluagribusiness@gmail.com
Intagram: KALULUAGRIBUSINESS
Facebookpage: KALULU AGRIBUSINESS SOLUTIONS
0713014501 /0683937375

                                                

Habari zilizopita

KILIMO CHA KOROSHO

KILIMO CHA KOROSHO UTANGULIZI Korosho ni zao la biashara ambalo chimbuko lake ni Ureno na baadae mnamo karne ya 16 ndipo li...