Sunday, September 9, 2018

FAIDA ZA UFUGAJI WA KUKU

FAIDA ZA UFUGAJI WA KUKU
Fursa katika ufugaji wa kuku
Fursa ni changamoto au matatizo yaliyotuzunguka. Kwa maana nyingine ni vitu gani tunavipata kwa shida katika mazingira yetu ya kawaida. Tumekuwa tukipata shida sana kufahamu jinsi ya kujua fursa zilizotuzunguka kutokana na kutojua neno fursa lina maana gani hasa kwa mapana yake. Tukija katika sekta ya ufugaji wa kuku, fursa iliyopo ni changamoto tunazokumbana nazo kila siku katika ufugaji wa kuku aina zote. Tusilalamike kuwa hatuwezi kufanikiwa. Katika mazingira yetu kuku kazoeleka kama utamaduni wa kila kaya ya kitanzania kuwa na kuku lakini anachukuliwa kama mfugo wa kawaida asiye na faida yoyote, lakini kuku ni fursa kubwa ambayo imetoa watu wengi kiuchumi. Tutumie nafasi tuliyonayo kujikwamua kiuchumi.

Hizi ni faida za ufugaji wa kuku.
1. Kuanza na mtaji mdogo
 Hii ni moja kati ya faida za kuanzisha mradi wa kuku. Kwa kawaida mtu yoyote anaweza kuanzisha mradi huu wa kuku kwa sababu hauhitaji mtaji mkubwa ili kuanza. Mfano kuku mmoja ambaye ni mtetea ma jogoo mmoja unaweza kuanza kama mradi. Changanuo ufuatao unaonyesha ni kwa jinsi gani. Mtetea mmoja na jogoo unaweza kununua kwa elfu 25 kwa maana jogoo elfu 15 na mtetea 10, baada ya mwezi mtetea atakuwa ameanza kutaga na ndani ya mwezi. Kipindi amemaliza kutaga ukamuwekea mayai 10 na 15 ndani ya siku 21 atatotoa vyote au 10. Vifaranga 10 ukawalea mpaka miezi 6 watakuwa kuku wakubwa na baadaya hapo wataanza kutaga na kulalia na kupata vifaranga wengi na ukaendelea kupata kuku wengi zaidi. Ndio maana unaweza kutumia mtaji mdogo na baada ya kuwa na kuku wengi na kuanza kuuza.
2.Chanzo chan mapato.
Kuku ana bidhaa muhimu kama vile mayai,  nyama, na kinyesi ambacho hutumika kama mbolea ya asili. Vyote hivi ni mahitaji ya binadamu katika maisha ya kila siku. kupitia kufuga Kuku utapata fursa ya kutengeneza pesa nyingi tu. Kama utakuwa mfuatiliaji mzuri, kwa maana kuwapa chanjo kwa wakati, chakula bora na kutibu magonjwa pindi yakitokea. Kuku wa kienyeji aliyekoma anauzwa 15000, 20000, 25000, 30000 na kuendelea inategemeana na kuku mwenyewe. Tatizo kubwa tulilonalo Watanzania hasa kwa kuku wa kienyeji kadhalaulika na kuonekana ni wa kawaida lakini tukikaa kujua trei moja mayai ya kienyeji linauzwa 15000. Je? Ukiwa unaweza kuzalisha trai 5 kwa siku utakuwa na shilingi ngapi. Tuamke na kufanya ufugaji wa kuku kuwa wa uwakika.
3.Utawala wa mradi wa kuku ni rahisi.
 Urahisi huu hauna maana kuwa hakuna ugumu hapana ila maana kubwa ya hii pointi ni kwamba hatakama ni mfanyakazi wa kuajiliwa utapata muda wa kufuatilia kwa karibu maendeleo ya kuku wako. Mfano umeanza na mradi wako wa kuku 100 ,umewafugia nyumbani kwa kawaida unatakiwa kujipangia ratiba. Kwamba kabla ya kwenda kazi ni kufika bandani na kuwa hudumia kuku wako, hata kama utamwachia kijana aendelee kuwa hudumia kipindi ukiwa kazini, utakuwa unajua kuku wako wako salama. Pia jioni ukitoka kazini inabidi upate muda wa kipitia bandani na kuona hali ilivyo na kupata mrejesho kutoka kwa kijana uliyemwachia.
4.Soko la kuku ni kubwa Tanzania na nchi za nje pia.
 Hili swala ni fursa kubwa kwetu sisi vijana hasa ambao tumekuwa tukilalamikia kuhusu mambo ya ajira za serikali na mashirika binafsi. Lakini tazama watu wa nje ya nchi na baadhi ya wenyeji wanaoingiza bidhaa za kuku kama, vifaranga, kuku na mayai. Wakati nafasi ya kuzalisha hapa hapa tunayo ni swala la maamuzi na kuacha kulalamikia serikali juu ya ajira. Vijana ajira tunayo mikononi mwetu ni swala la kuchukua hatua. Uwezekano upo kwa Tanzania kuanza kujihidumia yenyewe na kuanza kutoka nje ya mipaka pia. Takwimu zinaonyesha bado hata nusu ya matumizi ya kuku kwa ndani ya nchi, Cha msingi ni sisi kutafuta taarifa sahihi ili kuweza kufanya maamuzi sahihi. 

Fuatilia machapisho mbalimbali na semina zinazotolewa na vijana wazoefu katika sekta ya kilimo na ufugaji kutoka KALULU AGRIBUSINESS SOLUTIONS ili uweze kuthubutu kujiajiri kupitia mradi wa kuku. 

TAMBUA
Mradi wa kuku ni benki hai.
Benki hai ni namna ya kuhifadhi pesa yako kwa matumizi ya baadae. Sasa ufugaji wa kuku ni benki hai maana yake ukiwekeza pesa yako katika kuku itakuwa sehemu salama na itaongezeka kwa kadri unavyozidi kuzalisha kuku wengi. Benki hii ni tofauti na benki za kawaida kwa sababu hakuna gharama yoyote ya makato ya uendeshaji, hapa ni kuhakikisha pesa yako inakuwa ni jitihada zako kuhakikisha unazalisha kuku wengi

No comments:

Post a Comment

Habari zilizopita

KILIMO CHA KOROSHO

KILIMO CHA KOROSHO UTANGULIZI Korosho ni zao la biashara ambalo chimbuko lake ni Ureno na baadae mnamo karne ya 16 ndipo li...